Social Icons



Ijumaa, 13 Machi 2015

UDAKU NA UMBEYA WA MASTAA WA BONGO;RAY, THEA NUSURA WAZICHAPE

WAIGIZAJI Vincent Kigosi ‘Ray’ na Salome Ndumbangwe Misayo ‘Thea’ nusura wazichape baada ya Klabu ya Bongo Movie Unit kumgeuzia kibao mwanadada huyo kufuatia kitendo chake cha kuanika uozo unaofanywa na ‘memba’ wa klabu hiyo. Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, kisa cha wasanii hao kumgeuzia kibao Thea ni kutokana na habari iliyochapishwa na gazeti ndugu la hili, Risasi Jumamosi iliyotolewa na mwanadada huyo  ikilaani vitendo vinavyofanywa na waigizaji hao vinavyoichafua tasnia ya filamu kwa jumla.
Chanzo hicho kiliendelea kudadavua kuwa kasheshe lilitokea mara tu baada ya Thea na mumewe Michael Sangu ‘Mike’ kuingia kwenye pati ya mtoto wa msanii mwenzao, Shamsa Ford ambapo mwigizaji Mayasa Mrisho ‘Maya’ alimrukia kwa kumkaribisha huku akimsifia na kumkumbushia alichokisema gazetini kuwa ni kizuri kinaweza kusaidia watu kubadilika.

 
Vincent Kigosi ‘Ray’.

“Maya alijifanya kumsifia sana Thea na kumwambia kuwa wasanii walikuja juu lakini yeye aliona ni sawa alichokisema ingawa kumbe alimsifia kwa unafiki kwani alipomuona Ray anatoka ndani akamgeuzia kibao na kuanza kuongea naye kwa kumgombeza,” kilisema chanzo.
Hata hivyo, chanzo kiliendelea kudai kuwa Maya alipoona hajasikika akamuita Ray na kumwambia kama amemuona mbaya wao Thea?
Ilidaiwa kuwa baada ya kuambiwa hivyo, ndipo Ray akamdakia Thea na kuanza kumlaumu akimwambia hakutegemea kama angetoa siri za chumbani kwenye vyombo vya habari kwa sababu anamwamini kama dada yake.
Ilifahamika kuwa baadaye Ray alianza kupaza sauti akitaka kumkwida Thea ambaye naye alipandwa na hasira huku akimwelewesha kwa kutoa maelezo ili kumshusha waongee kwa ustaarabu.

Michael Sangu ‘Mike’.
Hata hivyo, Maya, baada ya kuona amezua timbwili aliondoka eneo hilo na kuwaachia ‘soo’ wenyewe ambapo kama siyo Mike na wasanii wenzake, Deogratius Shija, Nikita na Rado damu ingemwagika.
Baada ya habari hiyo kujaa tele kwenye meza ya Ijumaa Wikienda, gazeti hili lilimtafuta Mike ambaye aliweka wazi kilichotokea na kudai kuwa Ray na Thea ni mtu na dada yake hivyo hawawezi kukwidana kwani mwisho walikaa na kuyamaliza

Wakamatwa na Viungo vya Albino Mwanza

Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limewakamata waganga wa kienyeji 55 wakiwa na viungo vya binadamu vikiwamo meno na nywele vinavyodaiwa kuwa ni vya watu wenye albino. Vitu vingine walivyokutwa navyo ni ngozi ya simba, nyumbu, mamba, vibuyu, njuga, vioo, shanga na debe tatu za bangi.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola, alisema waganga hao walikamatwa katika wilaya za Mkoa wa Mwanza kwenye msako ulioanza juzi. Alisema katika msako huo wamefanikiwa kuwakamata waganga hao wanaodaiwa kupiga ramli chonganishi zinazosababisha kuchochea matukio ya mauaji kwa albino na vikongwe.

“Katika msako wa Jeshi la Polisi ulioanza juzi tumefanikiwa kuwatia mbaroni waganga wa jadi 55 ambapo kati yao tumewakuta na nywele, meno za watu wenye albino waliouawa katika matukio tofauti mkoani hapa,” Mlowala.

Kamanda huyo wa Polisi alisema waganga hao watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili ikiwamo kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria pamoja na viungo vya binadamu.

Mbali na tukio hilo, taarifa kutoka wilayani Misungwi zinaeleza kuwa watu wanne wamefikishwa kortini mjini hapa kwa tuhuma za kuuza mafuta maalumu ya ngozi yanayotumiwa na watu wenye albino. Mafuta hayo yenye thamani ya Sh milioni tano, ambayo yalitolewa na Hospitali ya Bugando kwa watoto wenye albino wilayani humo.

Wanafunzi Wakutwa Wakilawitiana Katika Shamba la Migomba huko Moshi

Picha  Ya  Maktaba
Wanafunzi  wawili wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Ongoma iliyopo Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro wamekutwa wakilawitiana katika shamba la migomba jirani na shule hiyo.

 
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Jerad Kesi, amesema kuwa tukio hilo lilitokea Machi 5 mwaka huu.
 
Kutokana na tukio hilo, Mwalimu Kesi alisema mmoja wa wazazi wa watoto hao alivamia shuleni hapo na kuwapiga walimu kwa kile alichosema kuwa walimu hao walikuwa wamemdhalilisha mtoto wake.
 
“Siku ya tukio, wanafunzi wawili wa darasa la pili na mmoja wa darasa la kwanza walikutwa na mwalimu wangu wakilawitiana kwenye migomba.
 
“Walipojua mwalimu amewaona, walikimbia na kuacha nguo zao pamoja na yule wa darasa la kwanza. Tulipomhoji yule mtoto aliyebaki alikubali kwamba amekuwa akilawitiwa na kwamba ameshafanyiwa kitendo hicho kama mara saba hivi,” alisema Mwalimu Kesi.
 
Baada ya wanafunzi hao kutimua mbio, Mwalimu Kesi alisema walirudi nyumbani na baadaye mmoja wa wazazi wao alifika shuleni hapo na kuwashutumu walimu hao kwamba wamemdhalilisha mtoto wake kwa kumvua nguo.
 
“Baada ya majibizano kati ya walimu na mzazi huyo, mzazi huyo aliwapiga walimu kwa fimbo na kuwajeruhi.
 
“Kwa hiyo, nilichokifanya nilikwenda kutoa taarifa polisi na kupewa RB namba MJ/RB/988/15 kwa ajili ya kumkamata mzazi huyo,” alisema mwalimu huyo.
 
Naye Mwalimu Idda Kilawe ambaye ndiye aliyewakuta wanafunzi hao wakilawitiana, amesema kuwa siku ya tukio aliwakuta wanafunzi hao wakiwa ndani ya kibanda walichokuwa wamekijenga kwenye migomba.
 
“Niliwakuta wakiwa wamejenga kibanda cha miti na kukiezeka kwa matawi ya miti na ndani yake walikuwa wanafunzi watatu na wawili kati yao ndiyo walikuwa wakilawitiana.
 
“Nakumbuka siku hiyo nilikuwa natoka kuchukua matokeo ya mitihani na nilipokaribia eneo la tukio, nikasikia sauti za watoto. Niliposogelea eneo hilo niliwaona wanafunzi wawili wakiwa uchi na yule mdogo ndiye alikuwa amevaa sare. waliponisikia, wakakimbia,” alisema mwalimu Kilawe

TAZAMA PICHA ZA UCHAFU WAFANYAVYO WANAFUNZI WA VYUONI



































































Makalio Makubwa Yampaisha Chat Agness Masogange Marekani na Nigeria..

Staa  aliyejipatia umaarufu mkubwa kutokana na makalio yake, Agnes Gerald ‘Masogange’ sasa amepaa kimataifa zaidi na kuwa  gumzo hadi Marekani baada ya hivi karibuni mtandao mmoja wa watu maarufu nchini humo kumpa shavu.
Masogange aliripotiwa na mtandao wa Media Take Out na kumuelezea kuwa ni staa mwenye makalio makubwa barani Afrika akitokea Tanzania.Mbali na maelezo kibao ya kusifia wowowo lake, mtandao huo uliposti picha kibao za mwanadada huyo ambaye sasa anaishi Afrika Kusini akiweka mapozi tofauti ya kimitego.. Baada ya Mtandao huo Mkubwa kumuandika Mitandao mingine mikubwa ya Nigeria Kama Aquavibes nao walimuandika
Hata hivyo, baadhi waliponda maelezo hayo kwa kusema kuwa, Afrika ina mabinti wenye maumbo tata kuliko Masogange hivyo mtandao huo ungefanya uchunguzi kabla ya kuripoti habari hiyo

Aunt Ezekiel Akanusha Taarifa za Kujifungua

Aunty Ezekiel
Baada ya kuzagaa taarifa za staa wa filamu nchini Aunt Ezekiel kujifungua, mwanahabari wa GPL ametia timu nyumbani kwa Aunt na kujiridhisha pasipo na shaka kuwa mrembo huyo bado yu mjamzito na taarifa za kujifungua si za kweli.
Mitandao mbalimbali ya kijamii imeripoti taarifa za Aunt kujifungua kuanzia jana huku mingine ikimpongeza na kuweka kipande cha video kinachomuonyesha mwigizaji huyo akiwa ammbeba mtoto mchanga.
Kupitia akaunti yake ya Instagram, Aunt Ezekiel jana aliweka kipande cha video akiwa amembeba mtoto mchanga bila kuandika chochote ambapo mashabiki wake walimiminika na kuanza kumpongeza wakijua tayari kajifungua.
Akiongea na mwanahabari wa GPL Aunt amesema kuwa , hicho ni kipande cha mojawapo ya filamu yake aliyocheza siku nyingi. Na taarifa zilizoenea mitandaoni kuwa kajifungua si za kweli.
Kwa upande wa pili kijana anaesemekana ndio alimpa ujauzito huo, Mosesi Iyobo ambae ni mcheza dansi wa mwanamziki Diamond alibandika mtandaoni picha ya mama akiwa amebeba katoto (itazame hapo juu) na kupeleka watu kumpa pongezi pia.

Jumapili, 8 Machi 2015

Mkasa Mzima ilivyoanza Hadi Padri Feki wa Kikatoliki Kukamatwa Huko Morogoro Huu Hapa

Siri ya mafanikio ya Padri feki, Josephat Asenga, aliyekamatwa mkoani Morogoro, katika kuongoza Misa ya Kanisa Katoliki kwa kufuata taratibu zote maalumu bila kutiliwa shaka, imebainika.
Asenga aliyetumia vitambulisho feki, alipojitambulisha kwa uongozi wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Maria Madeko mkoani Morogoro, alipopewa fursa ya kuongoza Misa, alitekeleza wajibu huo wa kipadri bila kuacha shaka.
Akizungumza na mwandishi, kiongozi mmoja wa Kanisa Katoliki (jina limehifadhiwa), alithibitisha  kuwa Asenga alipofika Parokiani hapo kati ya Mei na Juni mwaka jana, hakutiliwa shaka hata kidogo kuwa si Padri.
Kwa mujibu wa kiongozi huyo, Asenga alifika kanisani hapo akiwa amevaa mavazi ya kipadri na kujitambulisha kuwa yupo nchini kwa mapumziko, akitokea nchini Marekani, alikodai ndipo anakofanyia shughuli zake za upadri katika Jimbo Kuu la New York.
Mbali na kuvalia mavazi ya kipadri, Asenga pia alionesha kitambulisho na kusababisha uongozi uamini kuwa ni Padri na kumpa makaribisho ya Padri mwenzao.
“Alipoonesha kitambulisho tulimwamini na jinsi alivyokuja na mavazi ya upadri na muonekano wake alionao, haikuwa rahisi kumtilia shaka,” alisema kiongozi huyo.
Baada ya kupata makaribisho ya kipadri, Asenga kwa mujibu wa kiongozi huyo, aliomba apangiwe zamu ya kuongoza misa ya Jumapili iliyofuata na kukubaliwa.
Kiongozi huyo alithibitisha kuwa Asenga aliongoza vyema misa hiyo, kwa kufuata taratibu zote za kanisa hilo kama zinavyofuatwa na mapadri wengine.
Kwa kawaida Misa katika Kanisa la Katoliki, huanzia  Sakestia, sehemu ambayo mapadri na waministranti, ambao ni wasaidizi wao, huvaa majoho na kusali kabla ya kuingia kanisani wakisindikizwa na nyimbo.
Baada ya kuingia madhabahuni, Padri hubusu madhabahu kabla ya kualika waumini katika Misa.
Mualiko huo hufuatiwa na maelezo kidogo na kuanza Ibada ya Kitubio, ambayo waumini hutubu dhambi zao na kujiweka tayari kusikiliza neno la Mungu.
Ibada ya kusomwa neno, kwa kawaida masomo matatu kutoka vitabu vya Agano la Kale na Jipya katika kitabu cha Bibilia Takatifu, Padri huanza kutoa mahubiri.
Mahubiri yakiisha, Misa huendelea kwa sadaka na baadaye, Padri huongoza waumini kuanza kukumbuka maelezo ya siku ambayo Yesu Kristo alitoa Sakramenti katika Chakula cha Mwisho kwa wanafunzi wake akitaka wamkumbuke.
Kwa kawaida, eneo hilo ndipo Padri kwa mamlaka aliyopewa, hufanya mageuzi ya sakramenti kuwa Hostia Takatifu, kwa maneno mengine hubariki mkate kuwa Mwili wa Kristo na divai kuwa Damu ya Kristo.
Kwa Wakatoliki, eneo la mageuzi ni eneo muhimu na ndio waumini hutuma maombi kimya kimya, wakiamini ndio Kristo anashuka mwenyewe.
Baada ya kutumikia Kanisa na kukubalika, Asenga aliaga kuwa anarudi nchini Marekani kwa kuwa muda wake wa mapumziko, umekwisha na kuagwa na Kanisa.
Wakati uongozi  wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Maria Madeko, ukiwa na imani kuwa Asenga ni Padri na amerejea New York, kuendelea na Utume, walipata taarifa za kushangaza kutoka kwa baadhi ya waumini, wakidai wamekutana na Asenga mitaani.
Mbali na taarifa hiyo ya kukutwa mitaani na waumini wake, taarifa zaidi zilieleza kuwa amekuwa akiishi na mwanamke katika eneo la Ujenzi, kinyume na desturi za mapadri wa Kanisa Katoliki duniani, ambao hawaruhusiwi kuoa.
Baada ya taarifa hizo, kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo, Asenga aliwekewa mtego na  Paroko wa Parokia hiyo ya Mtakatifu Maria Madeko, Malt Dyfrig Joseph.
Paroko huyo inadaiwa aliwaomba waumini wamshawishi Asenga afike parokiani hapo na baada ya kufika, alihojiwa na Paroko huyo na kudai kuwa alipata upadirisho katika Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Kamanda huyo, baada ya Paroko huyo kupata maelezo hayo, alifanya mawasiliano na Katibu wa Jimbo hilo la Dar es Salaam na kujibiwa kuwa hakuna jina la Padri huyo.
Mtego wa pili kwa mujibu wa Kamanda Paulo, ulifuata kwa Paroko huyo kutoa taarifa Polisi kuhusu uwepo wa Padri feki, ambaye aliaminiwa kwa kiwango cha kuruhusiwa kuongoza Misa.
Taarifa hizo zinasema Alhamisi ya wiki hii, saa 10:30 jioni, Asenga alimpigia simu Paroko huyo na kuomba ampangie kazi ya kuendesha Misa Jumapili ya leo parokiani hapo, na kukubaliwa ambapo Paroko huyo alimtaka afike kanisani.
Baada ya kufika, taratibu za kujulisha Polisi zilifanywa na askari walipofika kanisani hapo, walimkamata mtuhumiwa huyo.
Kwa mujibu wa Kamanda Paulo, baada ya kufanya mahojiano na Asenga, alikiri kuwa yeye si Padri na    walipokwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi, walimkuta akiwa na majoho saba ya upadri.
Taarifa zaidi tulizozipata jana, zilibainisha kuwa Asenga huenda kwa kutumia mbinu hizo hizo, alishaaminiwa kuongoza Misa katika mkoa wa Kilimanjaro katika maeneo ya Uru na Moshi na mkoani Singida.
Mbali na kukubalika katika mikoa hiyo, lakini taarifa zaidi zilibainisha kuwa Asenga alifanikiwa kote huko kuongoza Misa na kuaminiwa, kutokana na mafunzo ambayo aliwahi kupata huko nyuma.
Inadaiwa Asenga alianza kupata mafunzo katika Seminari ya Kanisa Katoliki ya Uru, ambako alipata mafunzo ya elimu ya sekondari.
Baada ya kumaliza kwa mafanikio masomo yake katika seminari hiyo, alichaguliwa kujiunga na Seminari ya Kibosho, ambayo inatajwa kuwa maalumu kwa ajili ya kutoa elimu ya falsafa kwa wanafunzi na wengi ni wanaotarajiwa kuwa mapadri.
Mafanikio aliyoyapata katika masomo ya falsafa katika Seminari ya Kibosho, yalimwezesha kujiunga na  Seminari ya Kipalapala, ambako inaelezwa ndiko kunakotolewa mafunzo ya Liturgia, ambayo nayo ni sehemu ya mafunzo wapewayo wanafunzi wanaotarajiwa kuwa mapadri.
Ingawa taarifa za mafunzo aliyopata zinatiliwa shaka, lakini namna alivyoongoza Misa bila kutiliwa shaka, imesababisha baadhi ya waumini kuanza kumjadili, ili kufahamu hasa nia yake ilikuwa ipi.
Kutokana na taaluma nyingine aliyonayo ya uhasibu, amesababisha baadhi ya waumini kuunganisha matukio na uwezo wake na kuamini kuwa huenda hakuwa akitafuta  sadaka.
Mmoja wa waumini aliyezungumza nasi kwa sharti la kutotajwa jina, alidai kuwa huenda Asenga alikuwa na njama za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa wafadhili mbalimbali.
Kwa mujibu wa madai ya muumini huyo, watu wa aina ya Asenga, ambaye ana taaluma na uwezo wa kipadri, wana njia nyingi za kujipatia kipato, hivyo inawezekana alidanganya wafadhili wake kuwa yeye ni Padri ili apate ufadhili huo.
Muumini huyo alikwenda mbali na kudai huenda masharti ya ufadhili huo, ni kupata picha au sauti yake akiongoza Misa kanisani.
“Inawezekana kuna mahali aliomba ufadhili kwa ajili ya kitu fulani na aliwadanganya kuwa yeye ni Padri, ndio maana akaamua kuomba zamu ya kuongoza Misa.
“Utapeli umeingia mpaka kwenye nyumba za ibada kweli? Wanadamu tumekosa hofu ya Mungu!” Alihoji muumini huyo na kuasa jamii kuwa macho, kwa kuwa hivi sasa matapeli ni wengi na kila siku wanatoka na mbinu mpya.

I am Still a V!RG!N and am Waiting for the Right Girl, ERIC OMONDI Reveals

Eric Omondi has rubbished rumours on social media and said today that he is not a father to any child and that he has never had s*x in his lifetime.

Eric told a local daily that he is still a v!rg!n and he is waiting for the right girl to lose his v!rg!n!ty to. He said this when he was asked if he was the father of Citizen TV’s Jacque Maribe’s son.

LULU Michael na Madai ya Kulipwa Mil.15 Kwa Kucheza Movie Moja



Sidhani kama kuna producer apa bongo mwenye kifafa cha akili, ambaye ataweza kumlipa LULU mil 15 kwa movie moja tu. Ki Ukweli  hakuna movie yeyote aliyowahi kuigiza LULU na kuweza kuvunja rekodi ya mauzo kuliko filamu nyingine yoyote hapa nchini na kuweza kuwashawishi ma producer kuweza kumtumia kwenye movie zao ata kwa dau la mil 5 tu.

Nina uhakika LULU anaweza kuongoza kwa mauzo ya magazeti ya udaku apa nchini, ila sio kwenye filamu za kibongo, huo ndio ukweli.

Siwezi kumlipa Shamsa ford (CHAUSIKU) laki Mbili na nusu kwenye movie ya CHAUSIKU then nikamlipe LULU mil 10 akaigize FOOLISH AGE, that is foolish.

Ni upuuzi kumlipa RIYAMA ALLY laki tatu kucheza filamu ya FUNGU LA KUKOSA nikamlipe LULU mil 6 kucheza movie ya FAMILY CURSE.

Ni laana kumlipa ODAMA (Jennifer kyaka) laki tatu kucheza filamu ya ODAMA ukamlipe LULU mil 8 kucheza movie ya FAMILY DISASTER.

Hakuna awezaye kumlipa NISHA (salma jabu) laki moja na nusu kucheza filamu ya ZENA NA BETINA ukamlipe LULU mil 20 kucheza movie ya HOUSEBOY.

Simaanishi kuwa LULU sio muigizaji mzuri ila kiwango chake kwenye tasnia ya filamu bado sana , she has a long way to go, asifananishe umaarufu Wa kwenye magazeti na mitandao ya kijamii na kiwango cha uigizaji wake kwenye tasnia ya filamu.

Diamond Platinumz Akaliwa Kooni na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imemtaka meneja wake kutoa nyaraka zinazoonyesha Mikataba ya Diamond ndani ya siku saba (7). Inaelekea kuna jambo haliko sawa! ...

These Photos Of Diamond Platnumz Grabbing His Girlfriends B*uttocks Will Make You Feel Like Crying

The 34 years old and mother of three has been having such a great time with Diamond, at least based on what she posts on Instagram every day.
They say age ‘don’t matter’ when it comes to love; Diamond who is only 25 seems to have swept Zari off her feet this time.

Diamond and Zari Hassan were recently in Zanzibar for the holidays and from the pictures she is posting, it was all about what lovers do best.
Zari Hassan posted these pictures;herbehind being grabbed firmly  

FOOTBALL NEWS

 
Blogger Templates