Social Icons



Jumamosi, 25 Julai 2015

CHRIS BROWN ARUHUSIWA KUONDOKA UFILIPINO BAADA YA KUKAMATWA SIKU NA KUWEKWA KIZUIZINI KWA SIKU MBILI.


Baada ya kuzuiliwa kutoka nchini Ufilipino kwa siku mbili hatimaye Chris Brown kaachiwa huru na kuondoka salama kabisa… msanii huyo ambaye alikuwa mjini Manila kwa ajili ya show alizuiliwa kuondoka siku ya Jumatano kutokana na madai ya kuwa hakutimiza wajibu wake wa kimkataba kipindi cha Mwaka mpya kuingia 2015.


Licha ya kuachiwa huru Chris Brown alichukua time na kupost Twitter kusema hakuhusika na madai hayo na alitimiza wajibu wake wa kimkataba kwani alirudi kutoa show nyingine kufidia show aliyoikosa mwaka mpya.

>>> “Manila mmetisha sana, nawapenda sana…ishu iliyotokea sio ndogo na aliyehusika kufanya hivi inabidi atafutwe, jina langu limetumika na sikufanya CHOCHOTE!!”<<< Chris Brown.

Hakuna maoni:

FOOTBALL NEWS

 
Blogger Templates