Social Icons



Jumanne, 28 Julai 2015

SNOOP DOGG AKAMATWA SWEDEN KWA KOSA LA DAWA ZA KULEVYA...SOMA ALICHOKISEMA HAPA

                                                                     Snoop Dogg

Kusikia Rapper Snoop Dogg kukamatwa na Polisi kisa dawa za kulevya sio story mpya kabisa, stori ni kwamba jamaa alipokuwa kwenye show Sweden, baada ya kumaliza alikamatwa na Polisi wakati akiwa anajiandaa kurudi zake Marekani.
Snoop alikamatwa akihusishwa na kosa la kutumia dawa za kulevya
kitu ambacho ni kinyume cha Sheria za Sweden… baada ya kumfanyia vipimo vya Uchunguzi walimwachia baada ya vipimo kuonesha jamaa hakuwa ametumia dawa hizo.
Kiukweli jamaa alikasirishwa sana na hii ishu na anaona kama Polisi walionesha vitendo vya Kibaguzi kumkamata, baada ya hapo jamaa kaapa kwamba hatamani hata kidogo kurudi tena Sweden 

>>>> “Samahani sana mashabiki wangu wote wa Sweden, sitorudi tena kwenye nchi hii… Mtamshukuru Bosi wenu wa Polisi na wahusika wote wa Idara ya Polisi ila ndio nshamaliza” >>>> Snoop Dogg.

Hakuna maoni:

FOOTBALL NEWS

 
Blogger Templates